“Binadamu ni tofauti na malaika hawaishi kwenye virambo, mitaa, vitongoji, vijiji wala miji, wao hawana mizimu hawana uzao wa kizazi kama sisi binadamu, hawazaliwi wala kufa. Hawana haja kuoa au kuoana na kuzaa watoto, ambao inabidi walishwe. Anga na mbingu zote ni makazi na makao yao. Ziraili na Jibril hawana haja ya kushirikiana. Kila mmoja ana maisha yake na anaweza kuishi peke yake. Binadamu huzaliwa kizazi hadi kizazi, na ni asili yao kutegemeana, kila mmoja akimtegemea mwenzake, na ndipo huweza kulishana, kuleana na kutunzana.”
Share this post
Makuadi wa Soko Huria
Share this post
“Binadamu ni tofauti na malaika hawaishi kwenye virambo, mitaa, vitongoji, vijiji wala miji, wao hawana mizimu hawana uzao wa kizazi kama sisi binadamu, hawazaliwi wala kufa. Hawana haja kuoa au kuoana na kuzaa watoto, ambao inabidi walishwe. Anga na mbingu zote ni makazi na makao yao. Ziraili na Jibril hawana haja ya kushirikiana. Kila mmoja ana maisha yake na anaweza kuishi peke yake. Binadamu huzaliwa kizazi hadi kizazi, na ni asili yao kutegemeana, kila mmoja akimtegemea mwenzake, na ndipo huweza kulishana, kuleana na kutunzana.”